Wednesday, November 29

Manyanyaso yanayowakuta watoto, kinamama Kenya

Watoto wa mitaani Kenya
Shirika binafasi la Shofco ambalo linafanyia shughuli zake mjini Mombasa nchini Kenya katika eneo la mabanda maarufu kama Bangladesh, limekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia masuala ya kina mama na hasa watoto.
Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili VOA anaripoti kuwa shirika hili hasa linawasaidia watoto ambao hukumbwa na manyanyaso ya mara kwa mara.
Kundi hilo linadai kuwa manyanyaso mengi yanawakumba wale ambao wanaishi katika maeno duni katika mitaa hiyo ya Bangladesh na mara nyingine hukosa hata msaada unaohusika kuwaondolea madhila waliyo nayo.
Shofco ina wafanyakazi wa kujitolea ambao lengo lao kuu ni kuisaidia jamii pale kunapotokea dhulma yoyote katika jamii hizo husika. Mwandishi wetu alipata fursa ya kuzuru mtaa wa mabanda wa Bangladesh mjini Mombasa na kukutana na baadhi ya kina mama ambao wanazungumzia yale ambayo huwasibu katika maisha yao ya kila siku.

No comments:

Post a Comment