Tuesday, November 14

Vijana wasema Jenerali wa jeshi hana nguvu zozote Zimbabwe

Jenerali wa jeshi la Zimbabwe Constantino ChiwengaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionJenerali wa jeshi la Zimbabwe Constantino Chiwenga
Vugu vugu la vijana wa chama tawala cha Zimbabwe limemkosoa jenerali wa jeshi mwenye cheo cha juu zaidi nchini humo kufuatia kauli aliyoitoa kwamba jeshi linajiandaa kuingilia kati kumaliza mzozo wa ndani wa chama tawala cha Zanu-Pf..
Ameambia vyombo vya habari mjini Harare kwamba mkuu huyo wa jeshi haungwi mkono na jeshi lote.
Tayari chama cha upinzani nchini Zimbabwe MDC kimepuuzilia mbali kauli hiyo ya jenerali wa jeshi kikimtaja kuwa asiye na nguvu zozote.
Matamshi hayo yanajiri kufuatia hatua ya Chimwenga kutishia kufanya mapinduzi iwapo chama cha Zanu-PF hakitasita kuwafurusha wapiganaji wa uhuru katika chama hicho ambao wametofautiana na rais Robert Mugabe na mkewe Grace Mugabe.
Msemaji wa MDC Kuraoune Chihwaye alinukuliwa akisema:
''Hana nguvu zozote kumzuia Grace kuwatukana wapiganaji wa uhuru wa zamani''.
Rais Robert Mugabe na mkewe Grace MugabeHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Robert Mugabe na mkewe Grace Mugabe
Jumatatu, jeneral Constantino Chiwenga alisema kuwa mvutano juu ya askari wa zamani lazima usitishwe.
Kauli hiyo ilipokelewa na wengi kama iliyomlenga Emmerson Mnangagwa, ambaye alifutwa kazi kama makamu wa rais wa Zimbabwe wiki iliyopita .
Taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii ya habari zinaelezea kuwa magari ya kivita yalionekana yakielekea katika mji mkuu Harare.
Sasa inadhaniwa kuwa ni magari ya kivita yanayosafiri kutoka kwenye kambi za kijeshi kuelekea kwenye kambi ya walinzi wa rais nje ya mji mkuu.

No comments:

Post a Comment