Thursday, November 9

Simba anayeumwa ngiri afanyiwa upasuaji Ngorongoro

Madaktari wa wanyama wakimfanyika upasuaji
Madaktari wa wanyama wakimfanyika upasuaji Simba aliyekuwa na uvimbe mwilini mwake katika hifadhi ya Ngorongoro, Arusha jana.Picha na (WMU) 
Arusha. Madaktari wa Mifugo wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) kwa kushirikiana na wataalam wa Taasisi ya wanyamapori (TAWIRI) wametumia  saa matatu  kumfanyia upasuaji simba ambaye ni mgonjwa.
Simba huyo, ambaye alikuwa eneo la creta Ngorongoro,  amekuwa akiumwa na muda mwingi kukaa peke yake ambapo taarifa za awali zilieleza huenda alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Ngiri ambao umemsababishia uvimbe.
Upasuaji huo ulianza majira ya saa saba mchana hadi saa 10 ulikuwa ukiendelea kwa ufanisi mkubwa na mara baada ya kukamilika na madaktari kujiridhisha na afya wa simba hiyo, ataachiwa kujiunga na wenzake.
Ofisa Idara ya uhusiano katika Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, Nickson Nyange alikiri leo  kuanza kufanyiwa upasuaji simba huyo na kueleza hadi majira ya saa 10 ulikuwa unaendelea.
"Muda huu madaktari na watafiti wanaendelea na upasuaji kuokoa maisha ya simba huyu, ambaye amekuwa ni mmoja wa vivutio vya utalii katika hifadhi yetu" Amesema
Hata hivyo, amesema  madaktari na maofisa wa Mamlaka ya Ngorongoro na Tawiri  kesho, watatoa taarifa kamili za kitaalamu juu ya ugonjwa uliokuwa unamkabili Simba huyo.
Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Dk Maurus Msuha  alikuwa kwenye kikao na kueleza angetoa taarifa hiyo mara baada ya kikao hicho kukamilika.

No comments:

Post a Comment