Thursday, November 9

Nyaraka za Paradiso: Maswali kuhusu uchimbaji madini Afrika

Katanga mineHaki miliki ya pichaPREMIERES LIGNES
Image captionTimbo la Katanga nchini DR Congo
Moja ya makampuni makubwa zaidi duniani ilimpa mkopo wa dola milioni 45 mfanyabiashara ambaye awali alikuwa ametajwa kwenye ufisadi, na kumuomba atafute leseni za kuchimba madini katika taifa moja maskini eneo la Afrika ya kati, uvujaji unaojulikana kama "Nyaraka za Paradiso" umefichua.
Kampuni ya Glencore ya Uswisi ilitoa mkopo huo kwa bilionea raia wa Israel Dan Gertler, dalali maarufu ambaye alikuwa na uhusiano na watu wa vyeo vya juu katika serikali ya Jamhuri ya Demokrasi ya Congo mwaka 2009.
Bw. Gertler aliombwa kutafuta makubaliano mapya kwa kampuni moja ya uchimbanji madini ambayo Glencore ilikuwa na hisa nyingi.
Yeye na Glencore wanakana kufanya lolote baya.
Glencore walikubali kumlipa Dan Gertler dola milioni 534 ili kununua hisa zake zote nchini DR Congo mwezi Februari mwaka huu.
Ufichuzi huo mpya ulitolewa kwenye Paradise Papera, ambao ni uvujaji wa zaidi ya nyaraka milioni 13.4.
Glencore, mfanyabiashara wa Israel na migodi DR CONGO
Image captionGlencore, mfanyabiashara wa Israel na migodi DR CONGO
Taifa la Jamhuri ya Demoksrasi ya Congo imekumbwa na ghasia na ufisadi kwa miongo kadhaa hali ambayo imesababisha karibu nusu ya watu wake kabaki hali mbaya ya umaskini.
Lakini madini mengi ya nchi hiyo ni ya thamani ya milioni ya dola kila mwaka kwa wale wanaoweza kuyafikia.
Moja ya kampuni hizo ni Glencore, kampuni moja kubwa na madini ya Uswisi.
Kwa vipimo inachukua nafasi ya 16 kati ya kampuni kubwa zidi duniani.
Kwa miaka mingi Glencore imehusika na uchimbaji wa madini nchini DR Congo hasa kwa uzalishaji wa shaba nyekundu.
Kampuni hiyo inasema kuwa imewekeza dola bilioni dola 50 nchini DRC.
Miaka kumi iliyopita ilikuwa na asilimia 8.52 ya hisa katika kampuni inayojulikana kama Katanga ambayo ilikuwa na kibali cha kuchimba shaba nyekundi kusini mwa nchi.
Mwezi Juni mwaka 2008 bodi ya kampuni ya Katanga ambayo ilikuwa na afisa wa wa cheo cha juu ilikumbwa na habari ambazo hazikuwa nzuri
Glencore ni nani
Image captionGlencore ni nani
Serikali ya DRC chini ya Rais Joseph Kabila ilitaka kujadili upya leseni za uchimbaji madini.
Makubaliano yake ya kwanza yalikuwa ni dola milioni 135.
Nyaraka zilizo kwenye Paradise Papers zinaonyesha jinsi bodi ya Katanga ilihisi kuwa matakwa ya mamlaka za DRC hayangekubalika.
Kwa mara ya kwanza ni rahisi kujua jinsi wakurugenzi waliamua kuomba msaada wa mfanyabiashara raia wa Israeli Dan Gerter.
Glencore ilikuwa tayari imewekeza dola milioni 150 katika kampuni ya Katanga na pesa hizo zingepotea ikiwa haingechimba madini.
Kampuni iliyomilikiwa na serikali ya Gécamines, ilikuwa inataka dola milioni 585, ili Glencore iruhusiwe kuchimba madini ya shaba nyekundu
Wakati kama huo Glencore ilikubali kuipa mkopo kampuni iliyokuwa kwenye visiwa vya British Virgin Islands kwa jina Lora Enterprise dola milioni 45.
Lora Enterprises ilikuwa ikidhibitiwa na familia ya Gertler.
Makubalino ya mkopo huo yalikuwa ni ikiwa Bw. angeshindwa kufanikiwa kupata leseni mpya ndani ya miezi mitatu, Glencore ilikuwa na haki ya kurejesha mkopo huo.
Paradise Papers zinasema kuwa Bw Gertler alifanikiwa kwa haraka, Gecaminis ikaunguza pesa ilizokuwa ikiomba hadi dola milioni 140 na kuikolea katanga dola milioni 445.

No comments:

Post a Comment