Wednesday, November 29

Mhariri wa zamani Mwananchi afariki dunia


Dar es Salaam. Mhariri wa zamani wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Abdallah Yakuti amefariki dunia.
Alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam tangu Jumatatu Novemba 27,2017.
Rashid, mtoto wa kwanza wa Yakuti akizungumza kwa niaba ya familia amesema mazishi yatafanyika kesho Alhamisi Novemba 30,2017 saa kumi jioni katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
“Baba yetu alikuwa anasumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu lakini hali yake ilibadilika ghafla Jumatatu; tulimpeleka hospitali kwa matibabu lakini akafariki dunia. Msiba upo nyumbani kwa marehemu Mabibo na mipango ya mazishi inaendelea,” amesema.
Mbali na MCL, Yakuti alifanya kazi Idara ya Habari (Maelezo), Shirika la Habari Tanzania (Shihata), Daily News na New Habari Corporation.
Yakuti ameacha wajane wawili, watoto wanne na wajukuu wanne.

No comments:

Post a Comment