Sunday, November 26

Meya Ubungo akamatwa



Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob
Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob 
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), kimedai kuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob amekamatwa na polisi wakati uchaguzi wa mdogo wa Kata ya Saranga ukiendelea.
Akizungumza leo Jumapili, msemaji wa chama hicho, Tumaini Makene amesema haijulikani meya huyo amepelekwa kituo gani na kwa kosa gani.
Amesema Jacob aliapishwa kuwa wakala katika majumuisho ya uchaguzi wa Kata ya  Saranga hivyo alikuwa anahusika katika uchaguzi unaoendelea katika kata hiyo.
Makene amesema uongozi wa chama hicho unafuatilia ili kujua sababu za kukamatwa kwake na wapi alipo.
"Sasa kama mtu tunayemtegemea kuwa wakala kwenye majumuisho ya kuhesabu kura unategemea nini, hizi ni rafu ambazo mamlaka husika zinatakiwa kufuatilia," amesema.

No comments:

Post a Comment