Tuesday, November 14

Mama Kanumba asema Lulu atatoka, Kanumba hatarudi tena


Dar es Salaam.  Siku moja baada ya Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuhukumiwa kifungo cha kutumikia jela miaka miwili kwa kosa la kuuua bila kukusudia, mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mutegoa amesema wanaombeza kwa kuishukuru Mahakama wamuache kwa hakuna mwenye uchungu zaidi yake.
Jana baada ya Mahakama Kuu kumtia hatiani mwigizaji huyo na kumpa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela, Mama Kanumba aliishukuru Mahakama akisema imetenda haki jambo ambalo lilizusha gumzo wengi wakisema hakupaswa kufurahia adhabu hiyo.
Akihojiwa na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam jana Jumatatu baada ya hukumu kutolewa alisema anashukuru kwa kuwa haki imetendeka na kwamba atakwenda kumzika rasmi mtoto wake.

Hata hivyo, Mwananchi leo Jumanne amesema asibezwe kwa kauli hiyo kwa kuwa hakuna anayeujua uchungu anaoupata kila siku.
“Mimi sijui kama ninafurahia kama wanavyodai, waulize kwamba, yeye (Lulu) alipokufa mwanangu Kanumba alifurahia? Mimi ni mkristo, sipendi kuona baya likimfika binadamu mwenzangu, lakini Lulu ameenda miaka miwili jela na atarudi, je, mwanangu atarudi lini? nitamwona wapi tena? Amehoji.

No comments:

Post a Comment