Monday, November 6

Mahakama ya juu yasitisha uchaguzi wa rais Liberia

George Weah (L) and Joseph Boakai (R)Haki miliki ya pichaREUTERS/ EPA
Image captionGeorge Weah (kushoto) na makamu wa Rais Joseph Boakai
Mahakama ya juu nchini Liberia imeamrisha kusitishwa kwa duru ya pili ya uchaguzi wa rais kufuatia madai ya kuwepo udanganyifu ikiwa imesalia siku moja kabla ya uchaguzi.
Ilisema kuwa uchaguzi huo hautafanyika hadi tume ya uchaguzi ichunguze madai hayo.
Madai hayo yalitolewa na mgombea wa chama cha Liberty Charles Brumskine, ambaye alichukua nafasi ya tatu wakati wa uchaguzi wa kwanza.
Hakuna tarehe mpya iliyotangazwa baada ya tarehe 7 mwezi huu.
Aliyekuwa nyota wa kandanda George Weah na makamu wa rais Joseph Boakai, wanatarajiwa kumenyana katika duru ya pili.

No comments:

Post a Comment