Wednesday, November 29

Magufuli akosa kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Rais Kenyatta

Rais John Pombe Magufuli
Image captionRais John Pombe Magufuli
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amemtuma makamu wake wa rais kumwakilisha katika sherehe ya kuapishwa kwa rais Uhuru Kenyatta nchini Kenya.
Rais Magufuli ambaye awali alikuwa amethibitisha kuhudhuria sherehe hiyo na hata kutuma taarifa kwa vyombo vya habari sasa amemtuma makamu wake Mama Samia Suluhu Hassan kumwakilisha.
Uhusiano kati ya Kenya na Tanzania umeonekana kudorora siku za karibuni hasa kufuatia kupigwa mnada kwa ng'ombe zaidi ya elfu moja kutoka Kenya waliokuwa wameingizwa Tanzania. Tanzania kadhalika ilichoma moto vifaranga waliodaiwa kutoka Kenya.
Tayari kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Edward Lowassa ambaye ni rafiki mkubwa wa rais Uhuru Kenyatta amewasili katika uwanja wa Kasarani tayari kwa sherehe hiyo.
Rais Magufuli ni mwandani wa karibu wa kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga ambaye alisusia uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26 ambao Uhuru Kenyatta aliibuka mshindi kwa kujipatia asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
Tayari makamu huyo anatarajiwa kuwasili katika uwanja wa Kasarani wakati wowote sasa

No comments:

Post a Comment