Saturday, November 11

Korea Kaskazini: Trump anachafua amani duniani

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Korea Kaskazini imemuelezea Rais Trump kuwa mchafuzi wa amani na utulivu wa dunia, ambaye anatamani vita vya nuklia vitokee.
Wizara ya mashauri ya nchi za nje ya Korea Kaskazini, imekariri nia ya taifa hilo kubaki na silaha zake za nuklia, ikisema silaha hizo zinalinda heshima na uhuru wa nchi.
Matamshi hayo yanasadifiana na mazoezi makubwa ya manuwari za majeshi ya wanamaji, baina ya Marekani na Korea Kusini.
Hii ni mara ya kwanza katika mwongo mzima, ambapo manuwari tatu za Marekani zinazobeba ndege, kuhusika katika mazoezi hayo.
Akiendelea na ziara yake katika bara la Asia, Rais Trump mara kadha, ameionya Korea Kaskazini, kwamba mradi wake wa silaha za nuklia, ni tishio ambalo halitovumiliwa.

No comments:

Post a Comment