Saturday, November 4

Kitabu chenye utata kuhusu rais Zuma chapigwa marufuku Afrika Kusini

Kitabu chenye utata kuhusu rais Zuma chapigwa marufuku Afrika Kusini
Image captionKitabu chenye utata kuhusu rais Zuma chapigwa marufuku Afrika Kusini
Majasusi wa Afrikia Kusini wanataka kufutiliwa mbali kwa kitabu kipya chenye utata kuhusu madaia yua rais Zuma kujilimbikizia fedha kimakosa ,wakisema kuwa kitabu hicho kimajaa makjosa na kinakiuka sheria ya ujasusi.
Shirika hilo la ujasusi limetishia kwenda mahakamani iwapo wachapishaji wa kitabu hicho NP watakataa kukifutilia mbali kitabu hicho kwa Jina ''The Presidency Keepers''-Wale wanaomueka Zuma mamlakani na kutokwenda jela, kilichotungwa na mwandishi aliyeshinda tuzo la uandishi wa uchunguzi Jacques Pauw.
Kitabu hicho kinadai kwamba bwana Zuma kwa muda wa miezi minne alipokea mshahara kutoka kwa mfanyibiashara mmoja mbali na mshahara anaolipwa na serikali na kwamba hakuutangaza mshahara huo kwa watoza ushuru wa taifa hilo.
Baada ya nakala za kitabu hicho kuchapishwa siku ya Jumapili katika gazeti moja, msemaji wa bwana Zuma alitoa taarifa ,akikana makosa yoyote dhidi ya rais Zuma akidai kwamba alikuwa mwathiriwa wa kampeni mbaya ya kumchafulia jina.
Rais Jacob ZumaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Jacob Zuma
"Maswala ya ulipaji wa kodi ya rais hayana makosa '',ilisema taarifa hiyo.
Nakala za kitabu hicho zinauzwa kwa kasi huku raia wakijaribu kukinunua kabla ya kuisha katika soko.

No comments:

Post a Comment