Thursday, November 2

HITILAFU YA MFUMO WA KUPOKELEA GESI KINYEREZI I, TATHIMINI YAONYESHA MATENGENEZO MAKUBWA YANAHITAJIKA, MAFUNDI WAKO KAZINI: TANESCO


Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, TANESCO


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
TATHMINI iliyofanywa na Wahandisi wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), kufuatia mfumo wa kupokea gesi asili kwenye mitambo ya kufua umeme, Kinyerezi I jijini Dar es Salaam kupata hitilafu, imebaini matengeenzo makubwa yanahitajika kufanyika ili kuhakikisha mfumo unarudi katika ubora wake..
Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, iliyosambazwa kwa vyombo vya habari leo Novemba 1, 2017, imesema kufuatia mfumo huo kupatwa na hitilafu majira ya mchana Oktoba 32, 2017, hatua ya kwanza iliyochukuliwa na wataalamu wa TANESCO ni kuzima mitambo ili kuruhusu kazi ya usafishaji kuondoa gesi hiyo kufanyika.
”Baada ya usafishaji wa Mitambo kukamilika, matengenezo yalianza usiku wa kuamkia leo Novemba 1, 2017, kwa kutumia wataalamu wa ndani wa Shirika pamoja na Mkandarasi wa kampuni ya JACOBSEN ELEKTRO AS.” Taarifa hiyo ya TANESCO ilisema.
Taarifa hiyo iliendelea kusema, “Kutokana na ukubwa wa matengeenzo na uangalifu wa hali ya juu unaotakiwa katika kazi hii hususan suala la usalama wa mitambo pamoja na watumishi wa Shirika waliopo katika eneo la mitambo, hatua za tahadhari zimechukuliwa.” Taarifa hiyo ilisema.
Aidha taarifa imefafanua kuwa kutokana na Mitambo hiyo kuzimwa ili kuruhusu kazi ya marekebusho ya hitilafu hiyo kukamilika kwa wakati, kutakuwa na upungufu wa umeme katika maeeno mbalimbali ya nchi.
“Uongozi wa Shirika unawaomba radhi wateja wake na wananchi kwa ujumla kwa maeneo ambayo bado yanakosa huduma ya umeme katika kipindi hiki cha matengenezo hayo na tutaendelea kuwaarifu wananchi jinsi kazi ya matengenezo inavyoendelea hadi kukamilika kwake.” Taarifa hiyo ilisema

No comments:

Post a Comment