Thursday, November 9

Binti shujaa mbunifu wa Emoji iliyo na Hijab

Emoji ya Hijabu iliyobuniwa na binti wa miaka 15 wa Saudi Arabia
Image captionEmoji ya Hijabu iliyobuniwa na binti wa miaka 15 wa Saudi Arabia
Binti mmoja ambaye ni mwanamitindo wa kibinafsi ambaye ametajwa kama "mwanaharakati wa emoji" Rayouf Alhumedhi ameandikisha historia ya digitalI, kwa kuundwa kwa mchoro uitwao emoji ili kuwakilisha wanawake wanaovalia vazi la heshima kwa wanawake waislamu la hijab.
Rayouf anasema kuwa alichoshwa kwa kushindwa kujitambua katika majukwaa ya kimataifa katika picha na alama zake za vidole: ''Kujihisi kutengwa, sio uhalisia wa kweli.....ni kama jambo ambalo ningependa liwepo au ninaloweza lifanyike'.
Hadi pale kampuni ya Apple, ilipotoa emoji hiyo, sikujua ninavyohisi,....
Mimi nina kwenda kuwa mwenye furaha kubwa. Naweza hata kufa kwa furaha niliyo nayo....!"
Aliambia idhaa ya BBC ya The Cultural Frontline, kuhusu namna, kupitia kazi ya uchoraji wa grafiki na ubunifu wa kisasa, kupitia mtindo wa Aphee Messer, emoji hiyo ya hijabi ikazaliwa.
Msichana huyo raia wa Saudia anayeishi Ujerumani, amebuni emoji hiyo ya ijab kwa wanawake waislamu.
Rayouf Alhumedhi, ana umri wa miaka 15, na ametuma pendekezo hilo lake hadi kwa The Unicode Consortium, shirika moja la kibinafsi lisilohitaji faida yoyoye, ili emoji hiyo mpya ipigwe msasa, liundwe na kunakifishwa kabla ya kuanza kutumika.
Ikiwa itaidhinishwa, bila shaka itaanza kutumika mwaka huu wa 2017.
Kuna tofauti gani kati ya hijab, niqab and burka?
Mataifa kadhaa ya Bara Ulaya yanaendelea na mjadala wa mavazi ya kiislamu yanayofunika uso
Image captionMataifa kadhaa ya Bara Ulaya yanaendelea na mjadala wa mavazi ya kiislamu yanayofunika uso
Mapendekezo hayo yanatukia wakati ambapo mataifa kadhaa ya Bara Ulaya yanapoendelea kujadili swala la mavazi ya kiislamu yanayofunika uso, kutumika kwa namna yoyote ile.
Mjadala huo unafanyika, chini ya Uhuru wa ibada, usawa wa kijinsia mingoni mwa wanawake, utamaduni wa kisasa na hofu ya kuongezeka kwa ugaidi duniani hasa wahanga wa kujitoa kufa.

No comments:

Post a Comment