Monday, October 9

WATU 12 WAPOTEZA MAISHA KUFUATIA AJALI YA GARI NDOGO (HIACE) KUTUMBUKIA ZIWA VICTORIA, RAIS DKT MAHUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI


 Juhudi za kuopoa miili ya watu waliokuwemo kwenye gari hiyo ikiendelea.
 Baadhi ya Wananchi mbalimbali wakilishuhudia tukio hilo la kuzama kwa gari ndogo ya abiria (HIACE),ambalo  namba zake za usajili hazikuweza kutambulika mara moja,mara baada ya kuopolewa ziwani.
 Wananchi kutoka maeneo mbali mbali wakilifuatilia tukio hilo mapema leo Kigongo Feri jijini Mwanza
Globu ya Jamii imepokea picha na maelezo kadhaa kutoka kwa mdau aliyeko jijini Mwanza zikionesha na kueleza kutokea kwa ajali  jijini humo mapema leo,amesema kuwa ajali hiyo ni ya gari ndogo ya abiria Hiace ikiwa na ibiria imepitiliza na kutumbukia ziwa Victoria katika kivuko cha kigongo  feri -Busisi,Wilayani Misungwi na kusababisha vifo vya watu 12  na majeruhi wawili.

No comments:

Post a Comment