Wednesday, October 18

Uhispania yatoa vitisho kwa Catalonia huku mzozo wa uhuru ukiendelea

Spain's deputy prime minister Soraya Saenz de Santamaria speaks during a news conference at the Moncloa Palace in Madrid, Spain, 16 October 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionSoraya Sáenz de Santamaría alitoa onyo siku moja moja kabla ya siku aliyopewa Carles Puigdemont, kumalizika
Uhispania itachukua hatua za kufutilia mbali utawala wa Catalonia ikiwa kiongozi wake hataachana na hatua za kutafua uhuru, naibu waziri mkuu amesema.
Soraya Sáenz de Santamaría alitoa onyo siku moja moja kabla ya siku aliyopewa Carles Puigdemont, kumalizika.
Serikali ya Catalonia imesisitiza kuwa haiwezi kutekeleza matakwa ya Madrid baada ya kura iliyokumbwa na utata ya Catalonia.
Kumekuwa na maandamano kupinga kuzuiwa kwa viongozi wa vugugu la Catalonia.
Jordi Sánchez na Jordi Cuixart wanazuiliwa huku wakichunguzwa kwa uhaini - hatua ambayo upande ambao unataka uhuru unaiona kuwa iliochochewa kisiasa.
Wanaume hao walikuwa viongozi wakuu kwenye kura ya uhuru ya Oktoba mosi, ambayo Uhispania ilitaja kuwa iliyo kinyume na sheria
Waziri mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy, anajaribu kuchukua tahadhari lakini suala kuwa yeye na serikali yake wanajaribu kufuta utawala wa Catalonia ni ishara ya jinsi uhusiano umedhoofika.
Hata hivyo kiongozi wa Catalonia Carles Puigdemont yuko chini ya shinikizo kutoka kwa watu wenye ushawishi wanaotaka ashinikize zaidi uhuru.
Pia kuna shinikizo kutoka kwa wafuasi wa Rajoy na washirika kuwa za kumtaka achukue hatua mara moja na kutekeleza kipengee cha 155 cha katiba mara baada ya siku ya Alhamisi.

No comments:

Post a Comment