Wednesday, October 18

Rais Kenyatta aitisha maombi kabla ya marudio ya Uchaguzi

Rais Kenyatta aitisha maombi kabla ya marudio ya UchaguziHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Kenyatta aitisha maombi kabla ya marudio ya Uchaguzi
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa nchi itafanya maombi mwisho wa wiki hii kabla ya marudio ya uchaguzi mkuu wa wiki ijayo.
Taarifa ya Rais Kenyatta ilikuja baada ya afisa wa cheo ya juu kwenye tume ya uchaguzi nchini Kenya, kukimbia nchi akisema kuwa amekuwa akipokea vitisho vya kuuawa.
Roselyne Akombe aliiambia BBC kuwa marudio ya uchaguzi, hayaafikii matarajio ya uchaguzi ulio huru na wa haki.
Bw. Kenyatta alisema kuwa wakenya watatumia wikendi kwa maombi na maridhiano kabla ya marudio ya uchaguzi wa urais ambao utafanyika tarehe 26 mwezi Oktoba.
Mpinzani wake mkuu Raila Odinga alijiondoa kutoka kwa uchaguzi huo wiki iliyopita.
Hata hivyo Rais Kenyatta hakuzungumzia kujiuzulu kwa Bi Akombe.

No comments:

Post a Comment