Sunday, October 1

10 wafariki baada ya ndege ya kijeshi kuanguka DR Congo

Picha ya ndege ya kijeshi ilioanguka
Image captionPicha ya ndege ya kijeshi ilioanguka
Ndege ya kijeshi imeanguka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwaua abiria wote.
Maafisa wa maswala ya angani wamesema kuwa zaidi ya watu 10 wamefariki baada ya ndege hiyo kufeli kupaa vizuri kutoka uwanja wa ndege wa N'djili katika mji mkuu wa Kinshasa na kuanguka katika makaazi ya Nsele.
Haijabainika iwapo kuna watu wowote waliouawa ama kujeruhiwa ardhini.
Mkurugenzi wa uwanja wa ndege wa Kinshasa amesema kuwa ndehe hiyo ilikuwa ikibeba mizigo na kwamba haikuwa na abiria wowote.
Ripoti nyengine zinasema kuwa baadhi ya wanajeshi waliuawa.

No comments:

Post a Comment