Thursday, August 31

WASANII NGULI NCHINI KUPIMANA MABAVU DIMBA CONCERT TRAVELNTINE MAGOMENI


 Meneja Tukio wa Tamasha la Dimba Concert , Mwani Nyangasa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Tamasha litakalo wakutanisha Wakongwe wa Muziki wa Dansi nchini na bendi ya Msondo Ngoma katika ukumbi wa Traventine September 2 mwaka huu kwa kiingilio cha shilingi 10,000 na 20,000 kwa VIP.
 Mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi Tamasha la Dimba Concert , Jimmy Chika akifafnua namna bendi hizo zitkavyotoa burudani kwa mashabiki na wadau wa Muziki wa dansi watakaofika katika ukumbi wa traventine siku ya Jumamosi
 Msanii wa Mkongwe wa Muziki wa dansi nchini, Husein Jumbe akiwatoa hofu Mashabiki wake kuwa muziki wao bado upo juu
 Mwanamuziki wa Mkongwe wa Double M Sound ,  Mwinyjuma Muumini akijigamba kwa tambo kuwa siku hiyo patachimbika kwa hiyo mashabiki wote wasikose kuhudhuria Tamasha hilo
 Mpiga gitaa la solo wa siku nyingi , Adolf Mbinga akionesha namna atakavyocharaza nyuzi siku ya Tamasha la Dimba Concert siku ya jumamosi
 Mwanamuziki Juma Kakere akieleza namna watakavyoweza kukonga nyoyo za Mashabiki kupitia nyimbo zake kadhaa ambazo ziliweza kutamba
 Rais wa Vijana wa Muziki wa Dansi nchini , Nyoshi Elsadat akieleza namna atakavyoweza kutoa burudani kwa wadau wa muziki wa Dansi na Mashabiki watakaofika siku hiyo
 Wanamuziki wakongwe wakiwa katika mazoezi yao wakionyesha namna watakavyoimba siku ya Dimba Concert  siku ya Jumamosi
 Rais wa Vijana wa Muziki wa Dansi nchini , Nyoshi Elsadat akiimba mbele ya waandishi wa habari namna atakavyofanya siku ya Dimba Concert itakayofanyika Sept 2 mwka huu katika ukumbi wa Traventine Magomeni

Na Agness Francis,Globu ya Jamii.

Wanamuziki wakongwe wa Muziki wa Dansi nchini wametambiana kuoneshana uwezo wa kuimba siku ya Tamasha la Dimba Concert litakalofanyika katika ukumbi wa Traventine Magomeni Septemba 2 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja tukio tamasha la  Dimba Concert,Mwani Nyangasa amesema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kwa  Taifa muziki bendi kupambana na wanamuziki nguli wa Bendi ya Msondo ngoma.

“ Dhumuni la tamasha hili ni  kuendeleza muziki wa dansi hapa  nchini  kwa kutumia wasanii hawa wakongwe ili waweze kuonesha vijana,wapenzi na wadau kuwa muziki huu bado upo hai.” Amesema  Nyangasa.

 Nae msanii nguli nchini Hussen Jumbe ametanabaisha kuwa wadau na mashabiki wa muziki huo wafike kwa wingi siku hiyo pale Traveltine  septemba 2 mwaka huu ili kupata radha halisi ya muziki wa dansi.

Kwa upande wake  raisi wa vijana  sauti ya simba Nyoshi El Saadat, amewaomba mashabiki wa muziki huo kufika  kwenye tamasha hilo  na kuwaahidi kutowaangusha na kuwapa burudani ya kukata na shoka.

No comments:

Post a Comment