Wednesday, August 30

Mvutano kuhusu kufunguliwa kwa mitambo ya tume Kenya


Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Kenya imeendelea leo kwa siku ya pili katika mahakama ya juu zaidi ya taifa hilo, huku mahakama hiyo ikisikiliza hoja za upande wa washtakiwa.
Mapema Mahakama hiyo ilipokea malalamiko ya mawakili upande wa upinzani NASA kwamba Tume ya uchaguzi (IEBC) ilikataa kuwapatia wataalam wake wa teknolojia ya mawasiliano fursa ya kuchunguza mitambo ya data ya tume hiyo ilizotumiwa kuhesabu kura za urais, kama ilivyoagizwa na mahakama Jumatatu.
Upinzani umedai mitambo ya IEBC iliingiliwa ili kumpatia ushindi rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti, tuhuma ambazo tume hiyo imekanusha.

No comments:

Post a Comment