Wednesday, August 30

Kim Jong-un: Tutarusha makombora zaidi Pacific

Baraza la usalama la umoja wa mataifa UN limeishutumu Korea Kaskazini.Haki miliki ya pichaBBC SPORT
Image captionBaraza la usalama la umoja wa mataifa UN limeishutumu Korea Kaskazini.
Vyombo vya habari vya taifa hilo pia vilirejelea vitisho katika kisiwa cha Marekani cha Guam katika bahari ya Pacific ambacho imesema kinamiliki kambi ya uvamizi wa kijeshi ya Marekani
Kombora lililorushwa siku ya Jumanne lilipitia juu ya kisiwa cha Japan cha Hokaido na kusababisha hali ya wasiwasi wa kusalama huku raia wakitakiwa kujificha kabla ya kombora hilo kuanguka baharini.
Baraza la usalama la umoja wa mataifa UN limeishutumu Korea Kaskazini.
Likifanya kikao chake siku ya Jumanne usiku mjini New York , baraza hilo lilitaja urushaji huo wa kombora kama ''ukatili'' na kulitaka taifa hilo kusitisha majaribio yake ya makombora.
Lakini matamshi hayo hayakutishia vikwazo vipya dhidi ya Pyongyang.
Korea Kaskazini mara kwa mara imekuwa ikifanyia majaribio makonbora yake katika miezi ya hivi karibuni, licha ya kupigwa marufuku kufanya hivyo chini ya sheria za Umoja wa Matifa.
Kombora la hivi karibuni lililotengezwa ni lile la Hwasong-12 ambalo lilizinduliwa mapema siku ya Jumanne katika kituo kimoja karibu na Pyongyang.
Njia iliotumiwa na kombora hilo la Korea Kaskazini
Image captionNjia iliotumiwa na kombora hilo la Korea Kaskazini
Liliruka kwa umbali wa kilomita 2,700 lakini likaenda chini chini juu ya Hokkaido kabla ya kuanguka baharini yapata kilomita 1,180 mashariki mwa Japan.
Japan ilitoa tahadhari kwa raia wake wa Hokkaido kujificha.
Waziri mkuu Shinzo Abe baadaye alisema kuwa ni hatua ''isiokuwa ya kawaida, hatari na tishio kubwa''.
Kwa mara ya kwanza chombo cha habari cha Korea Kaskazini KCNA kilikiri kurusha kombora la masafa marefu juu ya anga ya Japan.
Vifaa vyengine vilivyoonekana vikipitia juu ya nga ya Japan vilidaiwa kuwa satlaiti.
Korea ksakzini imesema kuwa kombora hilo lililenga kujibu zoezi la pamoja la kijeshi kati ya Marekani na Korea Kusini ambalo linaendelea mbali na kuadhimisha makubaliano ya Japan-Korea 1910 ambalo lilipelekea jeshi la Japan kuondoka katika rasi ya Korea.
KCNA kilimnukuu kiongozi wa taifa hilo Kim Jong Un akisema kuwa kama vita vya ukweli, urushaji wa kombora hilo ni hatua ya kwanza ya kijeshi ya raia wa Korea katika bahari ya Pacific na hatua ya kutaka kudhibiti kisiwa cha Guam.
Bwana Kim ameagiza kurushwa kwa makombora zaidi yanayolenga eneo hio la pacific.
Bwana Kim ameagiza kurushwa kwa makombora zaidi yanayolenga eneo hio la pacific.Haki miliki ya pichaKCNA
Image captionBwana Kim ameagiza kurushwa kwa makombora zaidi yanayolenga eneo hio la pacific.
Korea Kaskazini imetishia kushambulia kisiwa cha Guam, ambacho kinamiliki kambi kubwa ya kijeshi ya Marekani ambapo raia takriban 160,000 wa Marekani wanaishi mapema mwezi huu.
Maafisa wa Marekani walisema kwa kuwa Korea Kaskazini imeshindwa kutekeleza tishio lake kufikia sasa ni wazi kwamba imeanza kuogopa.
Rais wa Marekani katika taarifa yake iliyotolewa na Ikulu ya Whitehouse, amesema kuwa ''ulimwungu umepokea tishio la Korea Kaskazini kwa sauti kubwa na bila tashwishi''.
''Utawala huu umeamua kutojali majirani zake, na wanachama wote wa UN mbali na kufanya vitendo ambavyo havikubaliki kimataifa'', alisema.

No comments:

Post a Comment