Wednesday, August 9

Magufuli aruka kihunzi cha kuongezewa muda


Rais John Magufuli amesema hawezi kukaa madarakani kwa miaka 20 kwa kuwa anaheshimu Katiba na kwamba kazi ya urais ni ngumu.
Magufuli amesema hayo leo Jumatatu, Agosti 7 katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga alipozungumza na wananchi na kuzindua stendi ya kisasa ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya siku tano mkoani Tanga.
Kauli hiyo ya Rais imekuja baada ya Mbunge wa Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani kusema kwa kuwa Magufuli anafanya kazi nzuri itakuwa vizuri akiongezewa hata miaka 20.
“Nadhani Profesa Maji Marefu unataka niishi miaka 20 zaidi na siyo kuwa rais kwa miaka 20 kwa kuwa sitafanya hivyo kwa kuwa naheshimu Katiba,” alisema.
.

No comments:

Post a Comment