Wednesday, August 16

Kamishna wa tume ya uchaguzi Kenya azuiwa Uwanja wa ndege

Kamishna wa IEBC Roselyn AkombeHaki miliki ya pichaIEBC TWITTER
Image captionKamishna wa IEBC Roselyn Akombe
Kamishna wa tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC Jumanne jioni alizuiwa kusafiri kuelekea nchini Marekani na kutolewa katika ndege aliyokuwa amepanda.
Roselyn Akombe alikuwa akielekea nchini Marekani kwa ziara rasmi ya kikazi wakati maafisa wa uwanja wa ndege wa JKIA walipomkamata kwa kukosa kibali cha kumruhusu kutoka nchini kutoka kwa mkuu wa maafisa wa umma.
Alizuiwa katika kituo cha polisi cha uwanja wa ndege kabla ya ubalozi wa Marekani kuingilia kati na kulazimu apalekwe katika anga ya serikali katika uwanja huo.
IEBC ilithibitisha kisa hicho ikisema kuwa Akombe alikuwa akielekea Marekani kwa ziara rasmi na alitarajiwa kurudi siku ya Jumapili Agosti 20.
Baadaye aliruhusiwa kuondoka baada ya mkuu wa maafisa wa umma Joseph Kinyua kuingilia kati.
Aliondoka nchini Kenya alfajiri ya siku ya Jumatano tarehe 16.
Akombe ni mmoja wa makamishna waliosimamia uchaguzi mkuu nchini Kenya ambapo rais Uhuru Kenyatta aliihifadhi kiti chake.
Upinzani nchini humo Nasa umepinga matokeo hayo na unatarajiwa kutoa mwelekeo kwa wafuasi wake siku ya Jumatano, Agosti 16.
Baadhi ya wafuasi wa muungano huo wamekabiliana na maafisa wa polisi wakipinga matokeo hayo.
Hatua hiyo imesababisha mauaji ya raia huku wengine wengi wakijeruhiwa.

No comments:

Post a Comment