Sunday, August 13

Japan imepeleka mtambo wa kutibua makombora

Mtambo wa kutibua makombora wa Marekani Thaad ukipelekwa Korea Kusini
Image captionMtambo wa kutibua makombora wa Marekani Thaad ukipelekwa Korea Kusini
Japan imepeleka mtambo wa kutibua makombora magharibi mwa taifa hilo kufuatia tishio la Korea Kaskazini kwamba itarusha kombora la masafa marefu katika kisiwa cha Guam nchini Marekani.
Mtambo huo kwa Jina PAC3 (Patriot Advanced Capability-3) umepelekwa katika eneo la shimane, Hiroshima na Kochi ambapo Pyongyang inasema kombora lake litapaa kabla ya kuanguka katika maji ya Guam.
Mtambo wa kutibua makombora wa Marekani Thaad ukipelekwa Korea Kusini
Image captionMtambo wa kutibua makombora wa Marekani Thaad ukipelekwa Korea Kusini
Jeshi la kulinda baharini la Japan limeripotiwa kutuma mtambo wa kutibua makombora katika bahari ya Japan likiwa na mfumo wa kufuatilia makombora ya masafa marefu.

No comments:

Post a Comment