Thursday, July 20

Taarifa

Kwa mujibu wa Chadema media
Mbunge wa Ubungo Mh. Saed Kubenea anahitajika kuripoti Polisi siku ya leo tarehe 20. 07. 2017 kutoa maelezo kwa malalamiko yaliyofunguliwa na Prof. Ibrahim Lipumba
Kuitwa kwake kumekuja baada ya wiki iliyopita kufanya mkutano na waandishi wa habari katika ofisi ya Mkiti wa Kanda ya Pwani akiwa pamoja na viongozi wa CUF inayoongozwa na Mkiti wa Kamati ya Uongozi Julius Mtatiro na Katibu Mkuu Maalim Seif na kutangaza operesheni inayoitwa Operesheni Ondoa Msaliti Buguruni (OMB).
Operesheni hiyo itaendeshwa kwa ushirikiano wa vyama vinavyounda UKAWA

No comments:

Post a Comment