Saturday, July 22

RAIS Magufuli: Wawekezaji Wakichelewa Kufanya Mazungumzo na Serikali Nitafunga Migodi yote nchini

Akizungumza na wananchi akiwa eneo la Kakonko,Kigoma,maghiribi mwa Tanzania,Rais Magufuli ameonya kufunga migodi yote iwapo wawekezaji wataendelea kuchelewa kwa ajili ya mazungumzo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara katika wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma ambapo yupo kwa ziara ya siku tatu. Amesema haiwezekani makampuni hayo yanaendelea kuwa kimya wakati wameshakubaliana kuanzisha mazungumzo haraka.

"Makampuni ya madini yaliyoahidi kukaa na serikali kuzungumza, wafanye haraka wakiendelea kuchelewa nitafunga migodi yote wanayomiliki" Rais John Pombe Magufuli

Wakati huo huo, Wizara ya Nishati na Madini ya Tanzania imesimamisha shughuli za utoaji leseni za utafutaji na uchimbaji madini, mpaka tume ya madini itakapoundwa na kuanza kufanya kazi rasmi.

No comments:

Post a Comment