Saturday, July 22

MUGABE Apania Kuwafunga Wabakaji Miaka 60 Jela

Serikali ya Zimbabwe imependekeza adhabu ya kifungo cha miaka 60 jela kwa watu watakaopatikana na makosa ya ubakaji watoto chini ya umri wa miaka 12 na walemavu nchini humo.

Kwa mujibu wa gazeti la 'The Herald'  la nchini Zimbabwe linasema kuwa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka 40 jela kitawahusu wale wote watakaokabiliwa na kesi za ubakaji kama hatua ya kukomesha unyama huo.

Rasimu ya mapendekezo ya kurekebisha Sheria ya Uhalifu, imefanyika baada ya kilio cha wananchi kufuatia kuongezeka kwa visa vya ubakaji nchini humo.

Takwimu za Kipolisi zinaonyesha kwamba, takribani wasichana 325 walibakwa kwa mwezi mwaka jana na wengi wao wakiwa na umri wa kati ya miaka 11 na 15 hali hiyo ikimaanisha kila siku matukio zaidi ya 11 ya ubakaji hutokea.

No comments:

Post a Comment