Saturday, July 15

Mrithi wa Mghwira Act-Wazalendo kufanya ziara mikoa saba

Kaimu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Yeremia
Kaimu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Yeremia Maganja, 
Dar es Salaam. Kaimu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Yeremia Maganja, anatarajia kufanya ziara katika mikoa saba nchini kwa ajili ya kukagua uhai wa chama na maandalizi ya uchaguzi wa ndani ya chama katika ngazi ya mitaa.
Taarifa iliyotumwa na kitengo cha mawasiliano cha ACT-Wazalendo, leo imeeleza kuwa ziara hiyo itaanza Julai 17 na mkoa wa kwanza utakuwa ni Mara.
“Katika ziara hiyo, Maganja atafuatana na katibu wa kamati ya kampeni ya uchaguzi Mohamed Massaga, pia watakutana na kamati ya uongozi ya mkoa na majimbo yote ya mkoa” imesema
Mikoa mingine itakayofikiwa katika ziara hiyo ni Simiyu (Julai 19), Shinyanga (Julai 20),Mwanza(Julai 21),Manyara (Julai 23),Arusha(Julai 24) na Kilimanjaro (Julai 25)
“Baada ya ziara hiyo na itakayofuatiwa na tathmini ya kina Mwenyekiti Maganja atamalizia mikoa iliyosalia ya Tanzania bara kabla ya kuelekea mikoani kwa ajili ya kujitambulisha rasmi,” imesema
Taarifa hiyo imesema ziara hiyo  itakuwa ni ya kwanza kwa kiongozi huyo ambaye alipokea kijiti cha uongozi kutoka kwa Mama Anna Mghwira, aliyeondolewa katika nafasi hiyo na kamati ya uongozi ya chama baada ya kuteuliwa na Rais John Magufuli kuwa mkuu wa  mkoa wa Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment