Tuesday, June 9

BALOZI AMINA SALUM ALI ATANGAZA KUWANIA URAIS


BALOZI wa kudumu wa Umoja wa Afrika (AU), 
huko Marekani, Mtanzania Amina Salum Ali,  

Balozi Amina ametangaza uamuzi wake huo mapema leo hapa hapa jijini Dar es Salaam.
Itakumbukwa ya kuwa Balozi Amina ambaye alidumu kwa muda mrefu kama waziri kwenye serikali ya Rais mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Salmin Amour Juma, almaarufu kama (Komandoo), aliwahi kutupa karata yake kuwania urais wa Zanzibar, kabla ya kujitoa.

Huyu anakuwa mwana mama wa kwanza kwenye historia ya chama cha Mapinduzi CCM, kutangaza kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hali kadhalika, Balozi Amina rekodi yake ya kwanza ni kuwa mwanamke wa kwanza kuwa balozi wa kudumu wa AU huko Marekani.

Mbali na kuwahi kuwa waziri, Balozi aAmina ndiyo muasisi wa taasisi ya Zanzibar Women Welfare Trust, inayojishughulisha na kupambana na afya ya akina mama na watoto hususan kwenye eneo la maambukizi ya VVU.

Kitaaluma Amina anayo shahada ya uchumi

No comments:

Post a Comment