Saturday, March 17

Varshita Staa wa maigizo Afrika Mashariki


Anatamba katika mchezo mpya wa kuigiza Varshita unaorushwa katika chaneli ya Maisha Magic East. Varshita ni zao la tamthilia pendwa ya Auntie Boss uliomtambulisha mwanamke huyu.
Kabla ya kuwa staa wa mchezo huo, alishiriki kutayarisha na kucheza kama mwigizaji mkuu wa Tamthilia ya Aunt Boss inayorushwa pia katika kituo cha telecisheni cha NTV cha nchini Kenya.
Ni mmoja kati ya mastaa wa maigizo Afrika Mashariki anayependwa kwa wakati huu. Eve D’souza, ndiyo jina lake halisi lakini Varshita ndio linalotambulika zaidi.
Varshita amezungumza na mwandishi wa Gazeti la Daily Nation, Hilary Kimuyu na kueleza mengi kuhusu sanaa ya maigizo, maisha yake binafsi na matatarajio yake.
Unajisikiaje kuwa Mkenya wa kwanza kuwa na tamthilia iliyotokana na tamthilia?
Nadhani hatujapata muda wa kutafakari kuhusu mafanikio hayo mimi na mwenzangu (Lucy Mwangi). Ilipoanza tamthilia ya Auntie Boss watu walikuwa wakitupongeza lakini kwa sababu tulikuwa bize tukiendelea kurekodi hata hatukupata wasaa wakujua kinachoendelea mtaani. Hata sasa nipo bize narekodi vipande vya Varshita kusema ukweli sipati muda wa kukaa kutafakari kwa sababu kila kunapokucha nipo kazini na ninafanya kazi mpaka usiku mkubwa.
Ni ipi tofauti kati ya tamthilia hizi mbili: Auntie Boss na Varshita
Waigizaji wakuu katika tamthilia ya Auntie Boss ni wafanyakazi wa ndani (House girl). Wazo la kutengeneza tamthilia ya Auntie Boss lilikuja baada ya mimi na rafiki yangu Lucy kuzungumza kwa saa mbili kuhusu visa vya wafanyakazi wa ndani tulivyokutanan navyo. Hapo ndipo tukaulizana kwanini tusitengeneze tamthilia ambayo wafanyakazi wa ndani watakuwa mastaa. Kuhusu kuanzisha tamthilia ya Varshita kulitokana na kinachoendelea katika Auntie Boss.
Unaweza kuona Varshita alivyoingia katika tamthilia. Ni mwanamke mkorofi, aliyejaa vituko na mwenye hila. Hata kwenye kurekodi Auntie Boss ilibidi watayarishaji wapunguze nafasi ya Varshita na Don kwa kuwa walikuwa waking’ara kuliko wahusika wakuu.
Lucy akasema hapana, inabidi tutenganishe stori ya hao watu wawili na kwa bahati nzuri tulipopeleka wazo letu Mnet walilifurahia sana.
Walifurahi kwa sababu hakukuwahi kutokea shoo yenye maudhui kama hii ya wapenzi wenye asili ya India na Kenya na kwamba kumekuwa na ubaguzi wa hali ya juu.
Varshita imepokelewaje?
Imepokelewa vizuri sana lakini kuna kitu kinanisumbua kichwa kwamba mashabiki wetu wengi ni watoto. Unakutana na mzazi anakwambia mtoto wangu anakupenda sana anasema akiwa mkubwa anataka kukuoa. Yaani watoto wanatuona kama katuni.
Una mpango wa kuzipeleka tamthilia katika filamu?
Varshita ilipoanza nilijisemea sipendi kutoa tatmhilia ndani ya tamthilia kama tulivyofanya kwa sababu nyingi ninazozifahamu hazikufanikiwa. Tulipokubaliana kutengeneza Varshita nilikuwa na wasiwasi sana huenda isifanikiwe. Ndivyo ninavyofikiri kwenye filamu. Sipendi filamu na kama itabidi kufanya hivyo tutatumia staili ya Bollywood.
Kuna uwiano wowote kati ya Varshita na maisha yako halisi?
Ninachopenda kucheza nafasi ya Varshita ni kwa sababu ni watu wa aina tofauti na mimi. Mimi ni mkimya nisiyependa migogoro na watu wala mabishano.
Varshita ni mkorofi, mimi ni mpole. Varshita hana huruma wakati mimi siwezi hata kusikiliza simulizi ya kusikitisha bila kutoa machozi.
Unautumiaji muda wa ziada?
Napenda kupika lakini kwa bahati mbaya napata siku oja tu ya kuwa jikoni. Ninafanya kazi kuanzia Jumatatu mpaka Jumamosi.

No comments:

Post a Comment