Friday, March 2

Tattoo ya Kale zaidi yabainika Misri

bcHaki miliki ya pichaTHE TRUSTEES OF THE BRITISH MUSEUM
Image captionMwili wa mwanaume aliyebainika kuwa na tattoo tangu miaka 5000 iliyopita alikufa na umri kati ya miaka 18 mpaka 21
Watafiti wamebaini michoro ya mwilini maarufu "tattoo" iliyokuwa mikongwe zaidi duniani ipo katika miili miwili iliyoishi miaka 5000 iliyopita huko nchini Misri.
Vielelezo vya michoro hiyo inaonyesha mchoro wa ng'ombe pori na kondoo katika upande wa juu wa mkono wa mwili wa mwanaume na bega la mwanamke
Ugunduzi huu unaweza kuondoa ushaidi wa kuwa shughuli hizi za kujichora mwili zilianza kufanyika barani Afrika miaka 1000 iliyopita.
Daniel Antoine, ni miongoni mwa waandishi wa tafiti hiyo katika makumbusho ya Uingereza inayotoa elimu ihusiyo habari zinazohusu asili na maendeleo ya binadamu wa awali na alisema ugunduzi huu unabadili mtazamo wa ueleo wa watu juu ya namna ya watu walivyoishi katika karne zilizopita.
Mwili wa mwanaume huyo uligunduliwa miaka 100 iliyopita.
Uchunguzi wa kitaalamu uliofanywa unaonyesha kuwa alikufa akiwa ana umri kati ya miaka 18 mpaka 21. Na kifo chake kilisababishwa na jeraha alilolipata mgongoni.
tatooHaki miliki ya pichaTHE TRUSTEES OF THE BRITISH MUSEUM
Image captionMmoja ulielezwa kuwa ni mchoro wa ng'ombe mwitu aliyekuwa na mkia mrefu na pembe kubwa,mwingine unaonekana kuwa ni kondoo mwenye pembe zilizopinda
Alama nyeusi katika mkono wake haukuonekana kama una umuhimu mpaka alipofanyiwa uchunguzi wa kielektroniki na kubainika kuwa mwili huo una tattoo ya wanyama wawili.
Mmoja ulielezwa kuwa ni mchoro wa ng'ombe mwitu aliyekuwa na mkia mrefu na pembe kubwa,mwingine unaonekana kuwa ni kondoo mwenye pembe zilizopinda.
tatooHaki miliki ya pichaTHE TRUSTEES OF THE BRITISH MUSEUM
Image captionTattoo inayoonyesha hali ya ujasiri na ujuzi na kutoa ujumbe Fulani wa kustaajabisha
Wakati picha ya mwili wa mwanamke unaonesha tattoo inayoonyesha hali ya ujasiri na ujuzi na kutoa ujumbe Fulani wa kustaajabisha.
Mwili wa mwanamke huyo wa kale una alama ya S ndogo nne zilizokuwa chini ya bega lake la kulia.
Mwanamke huyo pia alikuwa na alama inayowasilisha muziki unaotumika katika sherehe.
Mwili wa mwanamke una alama ya S ndogoHaki miliki ya pichaTHE TRUSTEES OF THE BRITISH MUSEUM
Image captionMwili wa mwanamke una alama ya S ndogo
Awali, Wataalamu wa watu wa kale walidhani kuwa ni wanawake peke yake ndio wana tattoo wakati wa miongo iliyopita lakini ushaidi uliobainika katika tattoo ya mwili wa mwanaume sasa unaonyesha kuwa uchoraji wa mwili ulikuwa unafanywa na jinsia zote.
Watafiti wanaamini kuwa tattoo zinaashiria ujumbe wa kutokuwa na hofu na ujuzi wa kustaajabisha.
Mifano kongwe ya tattoo iliyoonekana katika binadamu wa kale wanasadikiwa kuwa waliishi 3370 na 3100BC .

No comments:

Post a Comment