Friday, March 2

'Ninajipiga selfie 200 kwa siku'

Junaid AhmedHaki miliki ya pichaJUNAID AHMED/GETTY IMAGES
Junaid Ahmed anawafuasi 50,000 kwenye ukurasa wake wa Instagram na anakubali kuwa anapenda mno kujipiga picha (selfies)
kijana huyu mwenye miaka 22 anajipiga picha takriban 200 kila siku.
huziangalia picha zake kwenye mtandao wa kijamii zikipendwa na watu wengi, kama ikitokea zimependwa na watu chini ya 600 hufuta picha hiyo
''Nikiweka picha,ndani ya dakika moja au mbili huwa pengine inapendwa na watu 100. Ninajisikia vizuri"
Presentational white space
Utafiti uliofanyika hivi karibuni unasema hali hii ya kupenda kujipiga picha inaitwa 'Selfitis'.
Junaid, anaishi Essex,Uingereza, anasema amegundua ni namna gani mitandao ya kijaamii inaweza kuwa mibaya, lakini hachukulii jambo hilo kwa uzito.
'Unachokiona kwenye mtandao wa kijamii si kweli''.Anaeleza.
''Mitandao ya kijamii ni mizuri ukitumia kwa matumizi chanya.Lakini yasiathiri maisha yako kabisa kwa sababu unataka kuwa kama mtu mwingine kwenye mtandao wa Instagram...haina maana.''
Junaid is addicted to selfiesHaki miliki ya pichaJUNAID AHMED
Image captionJunaid anapendelea kujipiga picha ya 'selfie'
'Nilitaka kuonekana na mimi nimo'
Danny Bowman, 23,alikua akiweka picha zake za Selfie kwa wingi kwenye mtandao wa kijamii alipokuwa kijana mdogo.
''Nilitaka na mimi nifanane na hao ninaowaona, nikaona njia nzuri ni kuonekana vizuri'' alisema.
''Hali hiyo iliendelea, nikitumia saa kumi mbele ya kioo nikijipiga picha, kila siku''.
Danny took hundreds of selfies when he was 15 years oldHaki miliki ya pichaDANNY BOWMAN
Image captionDanny alijipiga mamia ya picha alipokuwa na miaka 15
Alipofika miaka 16 Danny alijaribu kujiua.
Alikwenda kwenye nyumba ya kubadili tabia ikagundulika alikua na tatizo la 'body dysmorphic disorder' na aliamini hali hiyo imesababishwa na kupenda sana mitandao ya kijamii.
Danny sasa yuko chuo kikuu anawasaidia vijana wadogo wenye matatizo ya akili.
Danny BowmanHaki miliki ya pichaDANNY BOWMAN
''Nakumbuka nilijiuliza nikiwa nimelala kitandani' ni namna gani nitaondokana na tatizo hili?' nikahisi kama hakuna namna.
''Picha ninazoweka sasa mtandaoni si za kujipia mwenyewe tena bali ni picha za mimi nikiongea na watu au nikitoa hotuba.
Taasisi moja ya masuala ya afya inatoa wito kwa serikali na majukwaa ya mitandao ya kijamii kutoa ujumbe wa tahadhari kwenye simu baada ya mtu kutumia mtandao kwa saa mbili, baada ya utafiti uliofanywa kuhusu madhara ya mitandao ya kijamii kwa vijana.
Inaelezwa kuwa kupenda kujipiga picha na kuweka mitandaoni zaidi ya mara sita kwa siku ni tatizo liitwalo Chronic selfitis,wamesema wataalam kutoka chuo cha Nottingham Trent na Thiagarajar nchini India.
Sasa Junaid anasema maoni mabaya dhidi ya picha zake mitandaoni havimsumbui tena kama awali, hata sura yake alikuwa akiibadilisha kwa sababu ya msukumo wa mitandaoni.
''miaka iliyopita sikuwa hivi, nilikua na asili yangu, lakini nafikiri kupenda sana mitandao kupita kiasi kuliniponza, nilitumia kamera kubadili kidevu, mashavu, midomo,macho, kichwani na kuweka tattoo na nyusi.

No comments:

Post a Comment