Saturday, March 17

Mama Kanumba azungumzia kumtembelea Lulu na tofauti zake na familia ya mwigizaji huyo


Mama wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, amesema anatamani kwenda kumuona mwigizaji Lulu anayetumikia kifungo cha miaka miwili jela lakini kwa bahati mbaya hawana maelewano na familia yake .
Akizungumza na gazeti hili amesema kama mzazi anaumizwa na hali anayopitia Lulu na angetamani kwenda kumuona ili kumpa moyo lakini ndio hivyo ndugu zake wanamuona kama yeye ndiyo kasababisha afungwe.
Amesema wanaomlaumu wanapaswa waelewe kwamba yeye alishasamehe kwani hata angefungwa miaka 100, haiwezi kumfanya Kanumba arudi.
“Tangu Lulu kahukumiwa nimekuwa nikipokea lawama na watu kunitusi kuwa mimi ndio sababu huku wakisahau kwamba mimi nilishasamehe kama binadamu na pia sio niliyekuwa mlalamikaji katika kesi hiyo isipokuwa alishatakiwa na Serikali, lakini yote namuachia Mungu kwani naamini kufungwa kwa msichana huyo hakuwezi kunirudishia mtoto wangu,” amesema.
Novemba 13, mwaka jana Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia mwigizaji mwenzake, kanumba.
Kauli hiyo ya mama Kanumba imepokelewa tofauti mtandaoni wengi wakinukuu kauli yake ya kusema anashukuru mahakama imetenda haki kwa kumpa adhabu ya kifungo binti huyo.

No comments:

Post a Comment