Wednesday, March 7

Hivi unafahamu umri sahihi wa kuanza kufanya mapenzi nchini mwako?

Mtoto aliyeolewa
Ufaransa inatarajia kuweka sheria maalum ya umri wa kuanza kufanya mapenzi kuwa ni miaka 15. Hivyo kufuatia mapendekezo hayo mtu yeyote atakayebainika kufanya mapenzi chini ya umri huo atakuwa amebaka.
Maamuzi haya yamekuja nchini humo mara baada ya madaktari na wanasheria kutoa ushauri wao kuhusiana na umri mtu anaostahili kuanza kufanya mapenzi.
Mabadiliko haya yamekuja kufuatia kesi mbili za hivi karibuni nchini Ufaransa zilizohusisha wanaume waliofanya mapenzi na wasichana waliokuwa na umri wa miaka 11.
Katika sheria ya sasa, kama mtu amekutwa na kosa la kufanya mapenzi na mtu chini ya miaka 15 iwe kwa hiari ama makubaliano, mshtakiwa atahukumiwa kwa kosa la kujamiana na mtoto lakini sio kosa la ubakaji.
Kosa hilo litamlazimu mshtakiwa kutoa kiasi cha dola 87,000 kama sehemu ya adhabu na kwenda jela miaka mitano.
Hukumu ni sawa kwa wanaofanya unyanyasaji kwa watu wazima na watoto lakini kosa la ubakaji huwa lina adhabu kubwa zaidi.
MacronHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Emmanuel Macron
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron anaunga mkono mpango huo wa kuweka kiwango cha umri wa kuanza kufanya mapenzi.
Mwishoni mwa mwaka jana, mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 30 alikutwa hana hatia baada ya ushahidi kueleza kuwa aliyefanyiwa vitendo hivyo hakuwa amelazimishwa wala kupewa vitisho vyovyote.
Hata hivyo wakati msimamo huo ukitolewa huko nchini Ufaransa hali ni tofauti katika maeneo mengine barani Ulaya. Sheria ya kujihusha na mapenzi inaruhusu katika umri tofauti;

Ulaya

Austria,Ujerumani,Italia ni miaka 14
Ugiriki, Poland, Sweden ni miaka 15
Ubeligiji, Netherland, Spain, Urusi na Uingereza ni miaka 16

Barani Afrika

Miaka 12; Angola
Miaka 13; Burkina Faso, Comoro, Niger
Miaka 14; Botswana (wanaume), Cape Verde, Chad (wasichana), Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (wasichana), Lesotho (wanaume), Madagascar na Malawi
Miaka 15; Guinea, Morocco
Miaka 16; Algeria, Botswana (wanawake), Cameroon, Ghana, Guinea Bissau, Lesotho (wanawake), Mauritania, Mauritius, Mozambique, Namibia, Senegal, Afrika kusini, Swaziland, Togo, Zambia, Zimbabwe.
Miaka 18; Benin, Burundi, Afrika ya kati,Ivory Coast, DRC (wanaume), Djibouti, Equatorial Guinea, Eritrea, Ethiopia, Gabon, Gambia, Kenya, Liberia, Mali, Nigeria, Republic of Congo, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Somalia, South Sudan, Tanzania, Uganda.
Miaka 20; Tunisia
Wakati ukatili wa kimapenzi kwa watoto ni kosa la jinai katika nchi nyingi za Afrika bado katiba za nchi hizo zimetoa mwaya kutokana na mila na desturi na kupelekea kuendelea kuwepo kwa mimba za utotoni na ndoa za utotoni.
Kwa mfano nchini Tanzania, ni hatia kwa mtu kujihusisha na mapenzi chini ya umri wa miaka 18 na kutajwa kuwa ni unyanyasaji kwa watoto na kinyume cha sheria.
Huku kuna mkanganyiko ambapo kwa mujibu wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaruhusiwa mtu kufunga ndoa akwa na umri wa miaka 14.
ukatili wa kimapenzi kwa watoto ni kosa la jinai katika nchi nyingi za AfrikaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionUkatili wa kimapenzi kwa watoto ni kosa la jinai katika nchi nyingi za Afrika
Nchini Kenya umri sahihi wa kuanza kujihusisha na mapenzi ni miaka 18 na yeyote aliye chini ya umri huo anatambuliwa kuwa ni mtoto. Ingawa ndoa pia inawezekana kufungwa katika umri huo, sheria haijaweka wazi.
Katika vigezo hivyo vya umri, Angola ikiwa ni nchi pekee ya barani Afrika iliyoweka umri mdogo zaidi ya watu kujihusisha na ngono, wa miaka 12.
Mara nyingi nchi nyingi barani Afrika huwa hawaweki wazi suala hili la umri wa kuanza kujihusisha na mapenzi kutokana na mila na desturi pamoja na imani za dini.
Na kwa upande wa Umoja wa mataifa hakuna sheria au muongozo maalum kuhusu umri ambao unaruhusu mtu kuanza kufanya tendo hilo, licha ywa kwamba kuna haki za kumlinda mtoto.

No comments:

Post a Comment