Monday, December 4

Marekani mbioni kukabiliana na tishio la Korea Kaskazini

National security adviser Lt. Gen. H.R. McMaster speaks at the FDD National Security Summit in Washington, US on 19 October 2017.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionHR McMaster anasema hakuna muda uliobaki kutatua tatizo lililopo
Mshauri wa masuala ya usalama wa Ikulu ya White House nchini Marekani, HR McMaster, amesema kuwa Marekani iko mbioni kukabiliana na tishio kutoka Korea Kaskazini
Uwezekano wa kutokea vita unaongezeka kila siku lakini vita sio suluhu pekee, aliuambia mkutano wa ulinzi.
Matamshi yake yanakuja siku tatu bqada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio lake la kwanza la kombora la masafa marefu katika miezi miwili kinyume na vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Kombora hilo lilipaa mbali na makombora mengine ambayo yalijaribiwa awali kbala ya kuanguka katika bahari ya Japan.
Haki miliki ya pichaKCNA
Image captionKombora la Hwasong-15 lilipaa mbali zaidi na makomboa mengine ya awali
HR McMaster ameitaka China kuiwekea vikwazo vya mafuta taifa hilo ili kufanya kuwa vigumu kwa Pyongyang kujaza mafuta makombora yanayofanyiwa majaribio.
Korea Kaskazini imeishutumu Marekani kwa kuchochea vita.
Imetaja zoezi la pamoja la kijeshi kati ya Korea kusini na Marekani kuwa la uchochezi na kwamba linaweza kusababisha vita.
Graphic: North Korea's high altitude tests
Image captionUwezo wa makombora ya Korea Kaskazini
Graphic: Possible range of missile fired on conventional trajectory
Image captionUwezo wa makombora ya Korea Kaskazini

No comments:

Post a Comment