Tuesday, December 5

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA AMZAWADIA MILIONI MOJA ASKARI WA KIKE KWA UTENDAJI KAZI MZURI KAZINI, JIJINI DAR


Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akimkabidhi zawadi ya Sh. Milioni moja(1,000,000) askari wa kike Sajini wa Magereza, Anna Akuny(katikati) kutokana na utendaji wake mzuri kazini aliouonesha katika Gereza la Wanawake Segerea(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(wa pili kulia) ni Mkuu wa Gereza Segerea, ACP. Godfrey Kavishe. 
Askari wa Kike Sajini Anna Akuny(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kulia) mara baada ya kumkabidhi zawadi ya utendaji kazi mzuri kazini. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza, Makao Makuu. 

Na Lucas Mboje, Jeshi la Magereza

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa ametowa zawadi ya utendaji kazi mzuri kwa askari wa Jeshi hilo Sajini Anna Akuny wa Gereza la Wanawake Segereza leo Desemba 5, 2017 katika Makao Makuu ya Magereza Jijini Dar es Salaam. Askari huyo Sajini Anna amekabidhiwa Sh. milioni moja (1,000,000) na Kamishna Jenerali wa Magereza kutokana na kuonesha utendaji wake mzuri pamoja na nidhamu kazini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa amemtaka askari huyo kutokubweteka na mafanikio hayo bali iwe chachu ya kufanya kazi kwa bidii zaidi. Jenerali Malewa ametoa wito kwa Maafisa na Askari wa Jeshi hilo kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na miongozo inayotolewa mara kwa mara na Uongozi wa Jeshi hilo.

Hafla ya kukabidhi zawadi kwa askari huyo imehudhuriwa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Makao Makuu, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, DCP. Augustine Mboje pamoja na Mkuu wa Gereza Segerea, ACP. Godfrey Kavishe.

No comments:

Post a Comment