Saturday, November 11

Sanamu ya Adolf Hitler yaondolewa katika jumba la makumbusho

Sanamu moja ya Adolf Hitler inayotumika sana kwa picha za ''Selfie'' na wageni katika makavazi ya Indonesia imeondolewa.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionSanamu moja ya Adolf Hitler inayotumika sana kwa picha za ''Selfie'' na wageni katika makavazi ya Indonesia imeondolewa.
Sanamu moja ya Adolf Hitler inayotumika sana kwa picha za ''Selfie'' na wageni katika makavazi ya Indonesia imeondolewa.
Picha zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii zinaonyesha watu wakitabasamu huku wakijipiga picha na sanamu hiyo katika lango la kambi ya Auschwitz.
Ni wakati jamii ya kimataifa ilipotoa hisia kali kuhusu sanamu hiyo ndiposa makavazi hayo ya De ARCA yalipogundua kwamba yamefanya makosa.
Makavazi hayo yalipo Jogjakarta, Java yalisema kuwa yalitaka kuwaelimisha watu.
''Hatutaki kuvutia hisia mbaya'', meneja wa operesheni za makavazi hayo Jamie Misbah, aliambia AFP.
Picha katika mitandao ya kijamii zinaonyesha watu kadhaa wakipiga picha na sanamu hiyo ikiwemo vijana wadogo waliovaa nguo za rangi ya machungwa wakipiga saluti ya Nazi.
Imewacha idadi kubwa ya watu duniani kuhisi vibaya licha ya makavazi hayo kusema kuwa hakuna mgeni aliyelalamika.

No comments:

Post a Comment