
Muuguzi mmoja ambaye alikamatwa baada ya kukataa kumruhusu polisi kuchukua sampuli ya damu kutoka kwa mgonjwa ambaye alikuwa amepoteza fahamu amekubali kulipwa fidia ya dola 500,000.
Alex Wubbels aliafikia makubaliano hayo na Manisapaa ya mji wa Salt Lake na chuu kikuu cha Utah, kwa mujibu wa wakili wake.
Kukamata kwake na polisi mwezi Julai kulizua ghadhabu baada ya video ya kisa hicho kuibuka baadaye. Anaonekana kuwa na pingu mikononi huku akilazimishwa kuingia katika gari la polisi .
Baadaye aliachiliwa bila ya kushtakiwa. Polisi aliyemkamata alifutwa kazi mwezi uliopita huku mkubwa wake akishushwa madaraka.
Polisi Jeff Payne alitumwa kwenda hospitali ya chuo cha Utah tarehe 26 mwezi Julai kuchukua sampuli ya damu kutoka kwa dereva ambaye alikuwa amehusika kwenye ajali ya barabarani na ambaye alikuwa amepoteza fahamu.

Mgonjwa hakuwa ameshukiwa kufanya lolote baya.
Bi Wabbels ambaye alikuwa katika zamu wakati huo alimuambia polisi Payne kuwa hakuwa na waranti ya kuchukua sampuli ya damu jinsi inavyohitajika na sera za hospitali na sheria za jimbo.
Pia alisema kuwa damu haingechukuliwa bila ya idhini ya mgonjwa.
Bi Wubbels alikataa kumuambia polisi alikokuwa mgonjwa au kumruhusu kuchukua damu.
Luteni James Tracy kisha akamuamrisha Det Payne kumkamata Bi Wubbels.
Hospitali ya chuo cha Utah baadaye ilisema kwa ilikuwa imeleta sera mpya zinazowazuia polisi kuingia hospitalini wenyewe kuchukua sampuli ya damu.
No comments:
Post a Comment