Wednesday, November 1

MAHAKAMA YAPOKEA HATI YA UKAMATWAJI ILIYOJAZWA KATIKA UPEKUZI ULIOFANYIKA NYUMBANI KWA WEMA SEPETU


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepokea hati ya ukamatwaji iliyojazwa katika upekuzi uliofanyika nyumbani kwa muigizaji maarufu wa filamu nchini, Wema Sepetu  kama kielelezo kwa upande wa mashtaka na kutupilia mbali hoja za upande wa utetezi zilizowasilishwa mahakamani hapo na wakili Peter Kibatala.

Uamuzi huo umetolewa leo, Novemba 1, 2017 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kusema kuwa upekuzi huo ulifanywa nyumbani kwa Wema na siyo Maungoni mwake kwani kama upekuzi ungefanyika maungoni mwake basi ni lazima angepekuliwa na askari wa kike.

Awali upande wa mashtaka ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula uliiomba mahakama ipokee hati ya ukamataji Mali uliofanyika nyumbani kwa Wema kama kielelezo huku upande wa utetezi ukipinga.

Kesi hiyo sasa itaendelea Novemba 16, mwaka huu. Huku Hakimu Simba akiagiza mashahidi wote wa upande wa mashtaka wafike siku hiyo.

Katika upekuzi uliofanyika nyumbani kwa Wema panadaiwa kuwa palikutwa na  misokoto inayodhaniwa kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.

Katika ushahidi uliotolewa na Inspekta Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Wille (43) kutoka ofisi ya Mkuu wa Upelelezi  wa Makosa ya Jinai Kanda Maalum ya  Dar es Salaam yeye alidai katika upekuzi huo walifanikiwa kukuta misokoto inayodhaniwa kuwa ni dawa za kulevya aina ya bangi.

Wema anashtakiwa pamoja na wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas. Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment