Saturday, October 21

Zitto asema ACT si jukwaa la kuisifia Serikali


Dar es Salaam. Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema chama chake siyo jukwaa sahihi la kuisifia Serikali kama wanachama wengine wanavyodhani.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi, Zitto amesema wanachama wanaodhani kama chama hicho ni jukwaa la kuisifia Serikali wajitathimini au kuchukua hatua kama wenzao walivyofanya.
Zitto amesema hayo ikiwa ni siku chache tangu aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho, Samson Mwigamba na wenzake kumi kuhamia CCM.
“Tulimwita Mwigamba katika kikao cha chama aje kutueleza kama tunakikuka misingi ya chama lakini hakufika. Chama kinaheshimu mchango wa kila Mwana-ACT, lakini tunawashauri wanaondoka wasiwashawishi wanachama wengine kuondoka,”
“Chama kimejiridhisha kwamba bado tunaendelea kusimamia misingi ikiwamo uzalendo sanjari na kupigania haki za demokrasia,”amesema Zitto
Amesema wanafanya yote hayo wakiongozwa na utu na uadilifu.
“Chama chetu kina ahadi tano ambazo ni kupambana na rushwa na ufisadi na kamati ya uongozi imebaini kama haijatoka katika misingi yake kama wengine wanaoondoka wanavyodai,”amesema Zitto.
Amesema bado wanaendelea kupambana na umasikini na hali ya maisha kwa Watanzania wote.
“Hatujawahi hata siku moja kwenda kinyume  na misingi ya chama hiki kama watu wanavyodai.”

No comments:

Post a Comment