Sunday, October 1

Uturuki yafungua kambi kubwa ya kijeshi Somalia

Kambi ya Kijeshi ya Uturuki nchini SomaliaHaki miliki ya pichaFACEBOOK/SOMALIA
Image captionKambi ya Kijeshi ya Uturuki nchini Somalia
Uturuki imefungua kambi kubwa ya kijeshi mjini Mogadishu, Somalia.
Hii itakuwa kambi yake kubwa kabisa ya mafunzo ya kijeshi nje ya nchi.
Kambi hiyo itayokuwa kando ya bahari, ina uwezo wa kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Somalia, zaidi ya 1500 kwa wakati mmoja
Lengo ni kulipa nguvu jeshi la Somalia, kupambana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Al Shabaab.
Wanajeshi zaidi ya 20,000 wa Umoja wa Afrika na wengine wa kigeni, wanapigana na Al Shabaab hivi sasa.
Kuna kambi kadhaa za majeshi ya kigeni nchini Somali.

No comments:

Post a Comment