Friday, October 6

Moto wateketeza soko la Gikomba, Kenya


Mchuuzi akijaribu kuokoa maliHaki miliki ya pichaAFP/GETTY

Mali ya thamani ya mamilioni ya pesa imeteketea baada ya moto kuzuka katika soko kuu la wazi nchini kenya, soko la Gikomba jijini Nairobi.
Moto huo ulizuka mwendo wa saa tisa usiku.
Ijumaa asubuhi, baada ya moto huo uliowaka kwa saa kadha kuzimwa, wachuuzi walikuwa wakichakura kutafuta bidhaa ambazo hazikuungua moto.
Soko la Gikomba ni miongoni mwa masoko makubwa zaidi Afrika Mashariki.
Wengi wa wachuuzi huuza nguo na bidhaa nyingine za mitumba.
Mmoja wa wachuuzi amemwambia mwandishi wa BBC Ferdinand Omondi kwamba amepoteza marobota 250 ya nguo ya thamani ya karibu dola 23,000 za Marekani (Ksh2.3m).
Chanzo cha moto huo bado hakijabainika.

Mabaki ya bidhaa
Kuzima moto
Wachuuzi
Mchuuzi akijaribu kuokoa mali
Mabaki

No comments:

Post a Comment