Monday, September 11

Watu 7 wauawa kwa kupigwa risasi Dallas Marekani

A video screengrab shows police vehicles arriving at the scene of the shooting in Plano, Dallas, TexasHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWatu 7 wauawa kwa kupigwa risasi Dalllas Marekani
Mtu mwenye bunduki amewaua watu saba kwenye nyumba moja mjini Dallas, Texas nchini Marekani, kabla ya kuuliwa kwa kipigwa risasi na polisi.
Watu wawili ambao nao walipigwa risasi wako hospitalini.
Msemaji wa polisi David Tilley alisema kuwa mshambuliaji aliuawa na polisi kwa kwanza ambaye alifika wakatin wa ufyatulianaji wa risasi. Polisi huyo hakujeruhiwa.
Kile kilichochangia shambulizi hilo bado hakijulikani au ikiwa mshambuliaji aliwafahamu waathiriwa.
"Tunajaribu kuangalia suala hili kwa kina," Bwa Tilley alisema.
Gazeti moja huko Dallas liliripoti kuwa wale waliouawa walikuwa wakitazama timu ya Dallas Cowboys, ambayo ni timu ya kandanda ya Marekani wakati walishambuliwa.
Polisi hawajatoa jina la mshambuliaji au muathirwa yeyote lakini wote wametajwa kuwa watu wazima.

No comments:

Post a Comment