Monday, September 11

Picha ya waziri mkuu wa Australia akishika mtoto na bia mkononi yazua maoni mitandaoni

Malcolm Turnbull kisses his young granddaughter while holding her in one hand and a beer in another, at a sporting match in Sydney on SaturdayHaki miliki ya pichaMALCOLM TURNBULL
Image captionPicha ya waziri mkuu wa Australia akishika mtoto na bia mkononi yazua maoni mitandaoni
Watu nchini Australia wamejitokeza kumtetea waziri mkuu Malcolm Turbull baada ya picha yake akimshika mjukuu wake na bia mkononi kuzungumziwa kwa wingi,.
Bwana Turbull alisambaza picha hiyo mwenyewe akimshika mjukuu wake kwenye uwanja mmoja wa kandanda mjini Sydney siku ya Jumamosi.
Picha hiyo ilichapishwa kwenye ukurasa wake wa Facebook.
Lakini ilizua maoni ya kumkosoa Bw Turnbul kutokana na kuwepo kwa bia.
"inakera kushika mtoto na bia mkononi," aliandika Marg Walker.
Suala hilo lilipata maoni mengi wakati lilianza kuangaziwa na vyombo vya habari.
Baada ya lawama kuibuka pia wale waliomtetea nao walinza kutoa maoni yao wakisema kuwa Bw. Turnbull hajafanya lolote baya.

No comments:

Post a Comment