Saturday, September 16

Kim Jong-un: Jeshi letu lazima liwe sawa na la Marekani

Rais Kim Jong un wa Korea kaskazini ameapa kwamba atahakikisha kuwa jeshi la taifa hilo lina uwezo sawa na ule wa MarekaniHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Kim Jong un wa Korea kaskazini ameapa kwamba atahakikisha kuwa jeshi la taifa hilo lina uwezo sawa na ule wa Marekani
Korea Kaskazini imetangaza kuwa lengo lake kuu kijeshi kwa sasa ni kuhakikisha inakuwa na uwezo sawa na Marekani.
Shirika la habari la Korea Kaskazini lilitoa taarifa hiyo baada ya kombora la majaribio la mwisho kufanywa, ikisema kuwa kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong-Un, amesema kuwa hataki kusikia Marekani ikisema itakabiliana na Korea Kaskazini kijeshi.
KIongozi wa taifa hilo Kim Jong un ameapa kuhakikisha kuwa taifa hilo linaafikia mpango wake wa kinyuklia kulingana na vyombo vya habari vya taifa hilo.
Lengo lake ni kuhakikisha jeshi la tifa hilo lina uwezo sawa na lile la Marekani kulingana na chom,bo cha habari cha KCNA kilichomnukuu kiongozi huyo.
Rais Kim Jong Un pamoja na maafisa wakuu wa jeshi wakisherehekea urushaji wa kombora jingineHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Kim Jong Un pamoja na maafisa wakuu wa jeshi wakisherehekea urushaji wa kombora jingine
Matamshi ya bwana Kim yanajiri baada ya taifa hilo kufanyia majaribio kombora lake kupitia anga ya Japan, likitajwa kuwa kombora lililosafiri kwa umabli mkubwa zaidi
.Hatua hiyo imesbabishwa mgawanyiko miongoni mwa mataifa ambayo yaliunga nyuma ya uMoja wa Matifa dhidi ya Korea kaskazini siku chache zilizopita.
Lazima tuyaonyeshe mataifa yaneye uwezo mkubwa vile taifa letu litakavyokamilisha mpango wake wa kinyuklia licha ya vikwazo visivyoisha, bwana Kim alinukuliwa na chamobo cha habari cha KCNA
Alisema kuwa lengo la Korea Kaskazini ni kuwa na jeshi lenye uwezo sawa na lile la Marekani ili kuwazuia watawala wa marekani kutotaja swala la kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Korea Kaskzini
Makombora ya Korea kaskazini yaliofanyiwa majaribio
Image captionMakombora ya Korea kaskazini yaliofanyiwa majaribio
Katika mkutano wa dharura, baraza la Usalama la umoja wa Mataifa, lilishutumu Korea Kaskazini kwa kufyatua Kombora juu ya Japan, lakini likasisitiza kuwa hakutakuwepo na vikwazo zaidi dhidi ya taifa hilo.
Awali Marekani ilionya kuwa Korea Kaskazini itashambuliwa kijeshi iwapo vikwazo ilivyowekewa havitatekeleza chochote.
Lakini Uchina kwa upande wake ilihimiza Marekani ikome kutoa vitisho na badala yake ianze kufanya mashauriano.

No comments:

Post a Comment