Saturday, August 26

Yingluck Shinawatra atorokea Dubai

Yingluck Shinawatra

Image captionYingluck Shinawatra
Taarifa kutoka Thailand zinasema aliyekuwa waziri mkuu Yingluck Shinawatra ametorokea Dubai baada ya kukosa kufika mbele ya mahakama kusomewa hukumu mjini Bangkok.
Vyombo vya habari nchini vinasema alitorokea kupitia Cambodia na Singapore, kabla ya kusafiri hadi katika taifa hilo la ghuba ambako kakake Thaksin - waziri mkuu wa zamani pia, anaishi uhamishoni.
Yingluck Shinawatra alikuwa anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 10 gerezani iwapo angepatikana na hatia ya uhalifu kutokana na kuzembea kazini katika kesi kuhusu mpango wa ruzuku kwa wakulima wa mpunga unaosemakana kuchangia ushindi wake katika uchaguzi.

No comments:

Post a Comment