Sunday, August 20

Dereva aliyewagonga na kuwaua watu 13 Barcelona asakwa na polisi

Younes AbouyaaqoubHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionAbouyaaqoub, 22, anaaminika kuwa mafichoni
Dereva ambaye alishambulia watu kwa kuwagonga kwa gari na kuwaua watu 13 mjini Barcelona, huenda bado yuko hai, na mafichoni kwa mujibu wa polisi wa Uhispania.
Polisi wanamtafuta Younes Abouyaaqoub raia wa Morocco, ambaye anatajwa na vyombo vya habari kuwa mshukiwa.
Mwanamume mmoja ambaye alitajwa kuwa mshukiwa mkuu Moussa Oukabir 17, ni mmoja kati ya wanaume watano waliouawa na polisi baada ya shambulizi huko Cambrils magharibi mwa Barcelona.
Ian Moore Wilson and his wife ValerieHaki miliki ya pichaVANCOUVER POLICE
Image captionIan Moore Wilson na mkewe Valerie waliuawa huko Las Ramblas
Polisi wanasema kuwa washukiwa walikuwa wakipanga mashambulizi mengine.
Walisema milipuko ya siku ya Jumatano kwenye nyumba katika mji wa Alcanar, uliwapokonya wapanga mashambulizi vifaa vya kutengeneza milipuko, kwa hivyo waliamua kufanya mashambulizi madogo wakitumia magari.
map
Image captionRamani
Abouyaaqoub, 22, aliishi mji wa Ripoll kaskazini mwa Barcelona. Watu watatu wamekamatwa mji wa Ripoll na mwingine huko Alcanar.
Oukabir awali alionekana kama mshukiwa mkuu lakini baadaye siku ya Ijumaa, mkuu wa polisi alikiambia kituo kimoja cha televiseni kuwa uwezekano kuwa alikuwa ndiye dereva ulikuwa mdogo.
(L-R) Moussa Oukabir, Said Aallaa, Mohamed Hychami and Younes AbouyaaqoubHaki miliki ya pichaAFP
Image caption(kushoto kwenda kulia) Moussa Oukabir, Said Aallaa, Mohamed Hychami na Younes Abouyaaqoub
Oukabir anashukiwa kwa kutumia stakabadjhi za nduguye kukodi gari lililotumiwa kufanya shambulizi la Barcelona na lingine ambalo lilitumika katika mji wa Vic kaskazini mwa Barcelona.
Mapema siku ya Ijumaa polisi waliwaua kwa kuwapiga risasi washambuliaji watano akiwemo Oukabir huko Cambrilis, baada ya wanaume hao kuendesha gari kwenda kwa wapita njia, na kumua mwanamke mmoja na kuwajeruhi watu wengine 6.
Map
Image captionBarcelona

No comments:

Post a Comment