Wednesday, August 23

ASILIMIA KUBWA YA WANANCHI WAISHIO VIJIJINI HAWANA ELIMU YA KUTOSHA

ASILIMIA KUBWA YA WANANCHI WAISHIO VIJIJINI HAWANA ELIMU YA KUTOSHA KUHUSU HUDUMA ZA MAWASILIANO -TCRA CCC

 Mjumbe wa Baraza na Mwenyekiti wa kamati ya Elimu na Uhamasishaji Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,John Njawa akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar kuhusiana na utafiti walioufanya kwa Watumiaji wa huduma za mawasiliano hivi karibuni wakishirikiana na Chuo cha Mipango cha Dododoma.Kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,Mary Shao Msuya na kushoto ni Mjumbe wa Baraza na Kamati ya Elimu Uhamisishaji -Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano (TCRA CCC),Nyanda Shuji
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano huo
 Mjumbe wa Baraza na Mwenyekiti wa kamati ya Elimu na Uhamasishaji Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano ((TCRA CCC)),John Njawa akitoa ufafanuzi kwa mmoja wa Waandishi aaliyeuliza swali kuhusiana na utafiti huo walioufanya,mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar.Kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,Mary Shao Msuya.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,Mary Shao Msuya pamoja na Mjumbe wa Baraza na Kamati ya Elimu Uhamisishaji -Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano (TCRA CCC),Nyanda Shuji (kushoto),wakionesha vitabu vyenye utafiti uliofanywa na Baraza hilo kwa Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano,wakishirikiana na chuo cha Mipango cha Dodoma.

 Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,Mary Msuya alisema kuwa utafiti huo umefanywa ikiwa ni moja ya mipango ya baraza hilo kwa mwaka 2016/2017.

Katika utafiti huo,Mary alisema kuwa utafiti huo ulifanyika katika wilaya tano,ambazo ni Manispaa ya Dodoma (Mjini),Chamwino (vijijini),Mvomero (vijijini),Temeke Manispaa (mjini),na Kaskazini A Unguja,Zanzibar (vijijini),alisema na kuongeza kuwa watu walioshirikishwa kwenye huduma hizo za mawasiliano ni 697,umri kuanzia miaka 15,huku asilimia 50.5 wakiwa wanafunzi wa elimu ya shule ya msingi. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji na Huduma za Mawasiliano,Mary Shao Msuya akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar kuhusiana na utafiti walioufanya kwa Watumiaji wa huduma za mawasiliano hivi karibuni wakishirikiana na Chuo cha Mipango cha Dododoma.

No comments:

Post a Comment