Thursday, July 20

TANZIA: MAMA WA MZAZI MWENZA WA MWANAMUZIKI DIAMOND PLATNUMZ AFARIKI DUNIA LEO


Mama mzazi wa Zarina Hassan maarufu kama ‘Zari The Boss Lady’ ambaye ni mzazi mwenza wa Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz, Halima Hassan (kulia) amefariki dunia asubuhi hii, baada ya kuugua kwa wiki kadhaa na kulazwa katika Hospitali ya Nakasero iliyopo nchini Uganda akidaiwa kusumbuliwa na maradhi ya moyo na figo.

Zari amethibitisha kifo cha mama yake kupitia ukurasa wake wa Instagram.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI..
AMEN.

No comments:

Post a Comment