Sunday, July 30

Neno La Leo: Ni Heri Kuwa Na Adui Mwerevu Kuliko Rafiki Mjinga....!

Image may contain: 1 person, sitting and outdoor


Ndugu zangu, 

Katika dunia hii tunayoishi, wakati mwingine ni heri mwanadamu ukawa na adui mwerevu kuliko kuwa na rafiki mjinga. 

Rafiki yako akitokea kuwa ni mtu mjinga, basi, naye atakushauri mambo ya kijinga. Na pengine asiwe na hata la kukushauri. 

Mwanadamu usikimbilie kumchukia adui yako, na hususan akiwa ni mwerevu. Yumkini kuna ya kujifunza kutoka kwa adui mwerevu.

Angalizo: Mwanadamu unapaswa pia kuusikiliza kwa makini ujinga wa rafiki yako mjinga. Yumkini katika ujinga wake anaokueleza, waweza ukaambulia moja au mawili ya kujifunza. Hivyo, usimdharau rafiki yako mjinga.

Ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa.

No comments:

Post a Comment