Friday, July 28

Lipuli yapewa fungu la usajili


Iringa. Aliyekuwa mgombea Uenyekiti wa Timu  ya Lipuli, Dk. Nuhu Muyinga ameikabidhi  Sh20 milioni alizoahidi kutumia kwa ajili ya timu hiyo kuweka kambi mkoani Iringa.
Muyinga alikabidhi fedha hizo kwa Makamu Mwenyekiti wa Lipuli, Ayoub Kiwelo katika makabidhiano yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Uwanja wa Samora mbele ya viongozi mbalimbali wa kamati ya utendaji wa timu ya Lipuli FC ‘Wanapaluhengo'.
Muyinga aliwataka viongozi hao kuzitumia fedha hizo kutumia kusajili wa wachezaji bora.
Alisema wakati wa kampeni za uchaguzi wa Lipuli aliwaahidi wanachama endapo watamchagua atatoa dola 20,000 kwa ajili ya kuirudisha timu hiyo nyumbani kuendelea na kambi ili wapenzi na wanachama waweze kushuhudia wachezaji watakaosajiliwa na timu hiyo.
Alisema kuwa baada ya kushindwa uchaguzi ameamua kutekeleza ahadi hiyo, lakini iende katika usajili wa wachezaji  na kuhaidi kuisaidia Lipuli iweze kufanikisha malengo yake.
 Makamu Mwenyekiti wa Lipuli FC, Ayoub Kiwelo alimshukuru kwa msaada huo na kumpongeza Muyinga kwa uzalendo wa kweli katika kuisaidia timu hiyo licha ya kushindwa katika uchaguzi.
Alisema kitendo alichoonyesha Muyinga ni cha kuigwa na kila mpenda soka mkoani hapa na kumwaahidi fedha hizo zitatumika kama ambavyo ameelekeza kwa uongozi licha ya kukabiliwa na changamoto nyingi katika timu ya Lipuli.

No comments:

Post a Comment